Friday 7 June 2013

(AUDIO) Nelly ft Future - Give U Dat

(AUDIO) Chris Brown ft Mario & Nicki Minaj - Somebody Else (Remix)

(AUDIO) Chamillionaire-Slow Loud & Bangin



(NEWS) TURK AFUNGUKA NA KUSEMA HAMJUI LIL WAYNE

   Turk amefunguka na kusema kuwa yeye hamfahamu Lil wayne wa sasa na kuwa anamjua zaidi lil wayne wa kipindi cha miaka ya nyuma.
   Turk ambaye alikuwa akiunda kundi moja na Lil wayne lilokuwa linakwenda kwa jina la Hot Boyz amesema tangu apate msala wa kukaa gerezani kwa kipindi cha miaka tisa kuna mambo mengi yamebadilika na kusema kama isingekuwa swala la kukaa gerezani angekuwa katika level ambayo anayo Lil wayne sasa kimziki.
  Turk amesema kuwa hivi sasa yupo katika movement ambazo zitamrudisha katika game ya muziki. Pia aliweza kuongelea swala linalomkabili Lil wayne la madawa ya kulevya na kusema hata yeye kipindi alivyokuwa na umri wa miaka 16 mpaka 17 alikua katika hali kama hiyo na alikuwa hamsikilizi mtu.

(NEWS) JE KUNA UWEZEKANO WA KUWEPO SEASON 3 YA WAWILI HAWA?

    Inawezekana wakawa wanatengeneza kitu ambacho ni special lakini wao hawakijui kwani kila kukicha kumekuwa na story mpya kati ya Chris Brown na mpenzi wake walie achana wiki chache zilizopita.
   Baada ya kuona tweets za kila mmoja akitumia muda kumlaumu mwenzie kwa kutengana kwao, sasa shughuli imehamia kwenye nyimbo. Chris ameachia nyimbo inayokwenda kwa jina la "somebody else" ambayo ukiisikiliza mashairi yake yanaonekana kulenga kabisa mahusiano yaliyovunjika kati yake na Rihanna.
  Kama haitoshi Rihanna nae amejibu mapigo kwenye nyimbo mpya ya Wale inayokwenda kwa jina la Bad(Remix) kwa kuimba chorus(kiitikio) kinachoonekana kujibu ngoma ya Chris Brown.
   Je kuna uwezekano kukawepo na season 3 ya watu hawa wawili?

(NEWS) MR NICE AHARIBU KENYA ATEMWA NA GRANDPA RECORDS

     Waswahili husema lisemwalo lipo kama halipo la jongea ndicho kilichotokea kwa Nice Lucas Mkenda maarufu kama Mr Nice, kulikua na story nyingi zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii kuwa Mr Nice ametemwa na kampuni ya Grandpa na producer na owner wa Grandpa records anaejulikana kwa jina la Rafiga amedhibitisha na kusema kuwa wameamua kutemana na Mr Nice.
   Owner huyo amesema wameshindwa kwenda sawa na Nice kwasababu alikua na mikataba mingine nje ya grandpa na wao wanaheshimu sheria na wakaamua ni bora kutemana nae. Lakini kwa story zilizoenea kitaani zinasema Mr Nice katemwa kutokana na kuwa mlevi, mgovi, na mpenda wanawake hivo kusahau majukumu yaliyompeleka Kenya.
   Inasemekana kuwa mshkaji amekosa zaidi ya shilingi milioni 140 kutokana na kuvunjika kwa mkataba huo, siku zote waswahili husema ukibebwa bebeka lakini ndugu yetu ameshindwa kubebeka