Baada ya kufanya kazi moja matata sana ambayo ilimrudisha upya katika game ya muziki JustinTimberlake ambayo alipigwa tafu na mkali Jay Z sasa wajipanga tena.
Justin alionekana akiwa na Jay Z pamoja na mkongwe mwingine kwenye game ya Hip Hop Nas Escobar wakiwa wanajiaanda kutengeneza nyimbo mpya ya pamoja na mzigo mzima wa kutengeneza ngoma hiyo utafanywa producer Timbaland.
Kama haitoshi siku za karibuni alionekana pia akiwa na Pharrell Wlliams wakijiandaa kutengeneza track. Kwa wale wanaoelewa shughuli ya Nas na Jay Z ambayo ikijumuishwa na Justin watakua wanafahamu nini kitakacho kuja.
Thursday 6 June 2013
(NEWS) WAKAZI WA MOROGORO WAPATA NAFASI YA KUUAGA MWILI WA NGWAIR
Leo wakazi wa mji wa Morogoro walipata nafasi ya kuuaga mwili wa aliyekuwa mwanamuziki wa kizazi kipya Albert Mangwea ambae alifariki wiki iliyopita nchini Afrika ya Kusini.
Shughuli nzima ilifanyikia katika uwanja wa Jamhuri na kisha mwili wa marehemu ukapelekwa nyumbani kwao Kihonda kwa ajili ya mazishi. Mungu aulaze mwili wa marehemu mahala pema peponi
Shughuli nzima ilifanyikia katika uwanja wa Jamhuri na kisha mwili wa marehemu ukapelekwa nyumbani kwao Kihonda kwa ajili ya mazishi. Mungu aulaze mwili wa marehemu mahala pema peponi
(NEWS) EMINEM AONEKANA STUDIO AKIWA NA BLACK HIPPY
Baada ya kuonekana mwezi uliopita akiwa studio na mchekeshaji maarufu Chris Rock na Big Sean leo mkali huyu wa miondoko ya hip hop ameonekana akiwa studio na crew ya Black Hippy.
Wakati wakiwa katika tour ya good kid m.A.A.d city pande za Detroit Black Hippy walipata nafasi ya kuwa pamoja studio na mkali huyu ambaye anajitayarisha kuachia album yake mpya na inasemekana crew hiyo itapiga collabo na mkali Eminem.
Wakati wakiwa katika tour ya good kid m.A.A.d city pande za Detroit Black Hippy walipata nafasi ya kuwa pamoja studio na mkali huyu ambaye anajitayarisha kuachia album yake mpya na inasemekana crew hiyo itapiga collabo na mkali Eminem.
Subscribe to:
Posts (Atom)